Social Icons

Monday 21 May 2012

RAIS KIKWETE ATEUA MAJAJI MAHAKAMA YA RUFANI


<><><>  
RAIS KIKWETE
































Rais Jakaya Mrisho Kikwete amewateua Majaji wawili wa Mahakama Kuu ya Tanzania kuwa Majaji wa Mahakama ya Rufani.
Taarifa iliyotolewa jioni hii na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam, imewataja walioteuliwa ni Jaji Semistodes S. Kaijage na Jaji Kipenka M. Musa.
"Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo, Jumatatu, Mei 21, 2012 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Y. Sefue, uteuzi wao ulianza tokea Machi 15, mwaka huu, 2012", taarifa hiyo ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, imesema kabla ya kuteuliwa kwake kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani, Jaji Kaijage (57) alikuwa Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam tangu Mei 17, 2007. Aliteuliwa kuwa Jaji Mahakama Kuu Novemba 28, mwaka 2000.

Naye Jaji Musa (57) alikuwa Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Tanga kabla ya kuteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.
Pia amewahi kuwa Wakili wa Serikali, Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba. Aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama Kuu Septemba 13, 2004.

No comments:

LATEST NEWS

Share

Widgets

 

Total Pageviews