Thursday, 29 November 2012
AIRTEL WAMKUMBUKA SHARO MILIONEA
Ben pol ft Lucci - majonzi
Wimbo huu ni mahususi kwa ajili ya Marehemu Hussein a.k.a Sharo Milionea aliyezikwa jana mchana huko kwao Muheza, Tanga Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Enter in GongaMx
Tuesday, 27 November 2012
Bonge la Bwana Ya Shetta Kutoka Wiki Ijayo Kwenye Radio Statio
Kama unaweza kukumbuka siku ya tarehe 25 mwezi huu msanii wa kizazi kipya ambae anazidi kufanya vizuri katika tasnia hii ya muziki wa hapa bongo maarufu kwa jina la Shetta, siku hiyo alikuwa akizindua au kuitambulisha track yake mpya aliyoipa jina la BONGE LA BWANA huku akisindikizwa na Roma Shilole,Young D,Ney wa Mitego,Nyandu Tozi,pasha,Stereo na wengine wengi ambao wote hao walikuja kumpa support katika uzinduzi wa hiyo ngoma yake.
Diamond Anyakua Tunzo Ya Msanii Bora Wa Kiume Nzumari Awards Kenya 2012.
KIFO CHA SHARO MILIONEA NI PIGO JINGINE 2012
Usiku wa jana ni ulikuwa usiku wa majonzi kwa watanzania wote hasa kwa waliokuwa mashabiki wakubwa wa msanii na mchekeshaji maarufu nchini Sharo Milionea,ambae amefariki dunia kwa ajali mbaya ya gari wakati akitoka Dar es Salaam kueleka wilayani Muheza, Tanga Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Tanga Costantine Massawe Hussein Ramadhani (Sharo Milionea) alikuwa akiendesha gari namba T478 BVR Toyota Harrier. Alipofika maeneo ya Segera gari lake liliacha njia na kupinduka mara kadhaa, likagonga mti nakusababisha kifo chake na yeye kutokea mbele ya kioo cha gari na kutupwa mbali.
Alisema Mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza Aliongeza kuwa hakuna kona kali wala ubovu wa barabara kwenye sehemu aliyopata ajali. Gari lake imehifadhiwa mahali salama kwakuwa limeharibika vibaya na kwamba kwenye gari alikuwa mwenyewe.
Habari kuhusu kuthibitika kwa kifo chake zilianza kuenea jana usiku ambapo kwa upande wa rafiki yake
wa karibu Kitale amesema alikuwa
akiipiga simu ya Sharo Milionea iliyokuwa ikiita kwa muda mrefu bila kupokelewa na kisha kupigiwa simu na Tundaman, Mzee Majuto na Mjomba wake Sharokumtaarifu juu ya kifo hicho. Naye Raisi wa Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) Bwana Simon Mwakifwamba alisema kwamba “Sisi binadamu tunaweza kuwaza hivi na Mungu naye akawaza lake kwahiyo sisi tunaziombea familia hizi Mungu azipe faraja ya kweli na nadhaniinatoka kwa Mungu,” alisema hayo kwenye kituo cha televisheni ya TBC.
Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie wamesema kuwa kifo cha Sharo Milionea kimetokea wakati ambao alikuwa ameanza kufanikiwa “Sharo umri wake na mambo aliyoanza kuyafanya ni makubwa. “Sharo alishaanza kupata matumaini yaani ni sawa sawa unatupa mbegu halafu uitegemee inaanza kuchepua Sharo alishaanza kuchepua,anachepua ile mbegu yake, ameanza kujisaidia yeye kama yeye sababu katika maisha lazima kwanza uanze kujisaidia wewe kama wewe halafu pili uingalie jamii inahitaji nini kwako. Amejipatia usafiri maskini ya Mungu, pa kulala, na maisha yote ya kutoka Dar es Salaam kwenda Tanga kuwaona wazazi kutumia gharama yake.”Maneno hayo yalisemwa na Bwana Steve Nyerere,na pia aliongeza na kusema kuwa Jmbo la msingi ni Kumwachia Mungu na kuondoa mawazo kuhusiana na kifo chake. Umoja wa wasanii wa filamu nchini umesema umepata pigo kubwa sana hasa kwakuwa bado wana msiba wa msanii mwingine wa filamu Marehemu John Stephano ambaye anatarajia kuzikwa leo. Wamesema baada ya mazishi hayo kesho wanatarajia kusafiri na mabasi mawili kuelekea wilayani Muheza kwaajili ya mazishi ya marehemu Hussein Ramandhani(Sharo Millionea).
GARI ALILOPATA AJARI NALO SHARO MILIONEA USIKU WA KUAMKIA LEO
Hilo ndo gari alilopatia ajali Marehemu Sharo Millionea hapo jana usiku akiwa anaelekea Tanga Muheza kumuona mama yake
Monday, 26 November 2012
BREAKING NEWZ-Source Tone Radio
Breaking Nuuz: Kwa habari tulizo zipata hapa punde katika meza yetu na zisizo na uhakika zinadai kwamba .Msanii wa Filamu na Vichekesho Sharo Milionea Amefariki kwa Ajali Muheza Tanga.Tutawapa taarifa zaidi.
Tuesday, 13 November 2012
RAISI KIKWETE ATETEA VYEMA KITI CHA UWENYEKITI WA CCM TAIFA HADI 2017
Are Humans Becoming Less Intelligent?
Wednesday, 7 November 2012
Malawi yasitisha sheria ya ushoga
Baadhi ya viongozi wa kimagharibi wametishia kusitisha kuzipa msaada nchi za Afrika ambazo zinakataa kutambua haki za mashoga
Ushoga ni haramu katika nchi nyingi za Afrika na linasalia kuwa swala tete katika jamii nyingi za Afrika zenye kukumbatia maadili ya kiafrika.
Mmoja wa viongozi wa kijamii wenye ushawishi mkubwa, bwana Kaomba, amiomba serikali kutoruhusu bunge kubadili sheria zake kuhusu ushoga. ''Hii ni kinyume na maadili'' alisema kiongozi huyo.
Mwandishi wa BBC mjini Blantyre Raphael Tenthani, anasema kuwa kusitisha kwa muda sheria hiyo, itawaudhi sana watu wengi hasa viongozi wa kidini pamoja na watu kwa ujumla.
Mnamo mwaka 2010, wanaume wawili walikamatwa na kushtakiwa kwa utovu wa nidhamu hadharani baada ya kusema kuwa wataoana.
Kesi hiyo ilivutia sana kero kutoka kwa jamii ya kimataifa na hata kusababisha baadhi ya wahisani kusitisha msaada kwa nchi hiyo, na ikawa pigo kubwa kwa nchi hiyo ambayo ni moja ya nchi maskini zaidi duniani.
Rais wakati huo akiwa , Bingu wa Mutharika - aliwasamehe wanaume hao kwa misingi ya kibininadamu ingawa alisisitiza kuwa ni kinyume na maadili ,na tamaduni za kiafrika na hata sheria za nchi.
Hata hivyo rais Joyce Banda, aliyemrithi Bingu aliwaambia wabunge kuwa anataka kubatilisha sheria hiyo na kuhalalisha mapenzi ya jinsia moja.
CHANZO;BBC SWAHILI
Rais akagua miradi 19 katika wiki moja
SHEREHE YA KUFUNGA MAONYESHO YA MOWE 2012 KATIKA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA JIJINI DAR
US ELECTS A PRESIDENT- IN PICTURE
Mitt Romney concedes defeat, congratulates Obama
President Obama's 2012 Victory Speech - Part 1
Tuesday, 6 November 2012
Obama wins second term, Romney concedes defeat
Barack Obama wins election for second term as president
Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Fadhil Soraga Amwagiwa Tindikali na Watu Wasiojulikana
BODABODA JIJINI MBEYA WAVAMIA KITUO CHA MAFUTA
Sunday, 7 October 2012
TUME YA KATIBA YAANZA AWAMU YA TATU
TUME ya Mabadiliko ya Katiba (kesho jumatatu,terehe8.Oktoba,2012) inatarajia kuanza awamu ya tatu ya kazi ya ukusanyaji wa maoni ya wananchi kuhusu KatibaMpya katika Mikoa tisa (9) ikiwemo saba (7) ya Tanzania Bara na miwili ya Zanzibar. Taarifa iliyotolewa (leo jumapili tarehe 7. Oktoba, 2012) Jijini Dar es Salaam, na Katibu wa Tume hiyo, Assaa Rashid na kusambazwa katika vyombo vya habari inaitaja Mikoa hiyo kuwa ni Mtwara, Kilimanjaro, Iringa, Singida, Njombe, Rukwa, Tabora, ambayo yote ni ya Tanzania Bara. Kwa mujibu wa taarifa hiyo inasema pia Tume hiyo inatarajia kuitisha mikutano yake katika mikoa miwili ya Zanzibar, ambayo ni Kaskazini Unguja na Kaskazini Pemba. Aidha taarifa hiyo inaongeza kuwa katika Mkoa wa Mtwara, Tumei taanza na Wilaya ya Nanyumbu, katika Mkoa wa Kilimanjaro Tume itaanza na Wilaya ya Moshi Mjini, katika Mkoa wa Iringa Tume itaanza katika Wilaya ya Mufindi. Kwa Mkoa wa Singida, Tume itaanza na Wilaya ya Iramba, wakati Mkoani Njombe , Tume itaanza na Wilaya ya Ludewa. Taarifa hiyo pia inaeleza kuwa katika Mkoa wa Rukwa Tume itaanzia katika Wilaya ya Nkasi, Mkoa wa Tabora Tume itaanza katika Wilaya ya Kaliua, Mkoa wa Kaskazini Unguja Tumeitaanza katika Wilaya ya Kaskazini “A” na Mkoa wa Kaskazini Pemba Tume itaanza katika Wilaya ya Wete. Tume hiyo pia inawaomba wananchi kuhudhuria mikutano itakayoitishwa na Tume na kushiriki kikamilifu katika kutoa maoni yao binafsi kuhusu Katiba Mpya. Taarifa hiyo pia inawasisitiza wananchi wamikoa hiyo hasa wanawake na watu wenye ulemavu kutumia fursa ya kushiriki katika mikutano hiyo inayoitishwa na Tume ili kutoa maoni yao kuhusu Katiba Mpya.








