Social Icons

Thursday, 27 September 2012

Phil Collins - Another Day In Paradise Lyrics

She calls out to the man on the street, "Sir, can you help me?
It's cold and I've nowhere to sleep. Is there somewhere you can tell me?"
He walks on, doesn't look back, he pretends he can't hear her
He starts to whistle as he crosses the street, seems embarassed to be there

Oh, think twice, it's just another day for you and me in paradise
Oh, think twice, it's just another day for you, you and me in paradise
Just think about it

She calls out to the man on the street, he can see she's been crying
She's got blisters on the soles of her feet, she can't walk, but she's trying

Oh, just think twice, it's just another day for you and me in paradise
Oh yes, think twice, it's just another day for you, you and me in paradise
Just think about it, uh - huh, just think about it

Oh Lord, is there nothing more anybody can do
Oh oh Lord, there must be something you can say

You can tell by the lines on her face, you can see that she's been there
Probably been moved on from everyplace, cause she didn't fit in there

Oh yes, think twice, it's just another day for you and me in paradise
Oh yes, think twice, it's just another day for you, you and me in paradise
Just think about it, uh - huh, just think about it

It's just another day for you and me in paradise
It's just another day for you and me in paradise
It's just another day for you and me in paradise
It's just another day for you and me in paradise
It's just another day for you and me, it's another day for you and me
It's another day for you and me in paradise
In paradise, oh, oh, oh, oh yeah


If you want to get more information about the background of this song, you can visit wikipedia (WiKi).

Tips to look for free audio clips
(Don't use those tips to download illegally. To buy music is always the best way to support your idols)

Use Google, Yahoo and MSN to find some auido clip sites. Sometimes search engines can direct you to right sites. Now that a lot of auido clip sites are banned by search engines, remember to make good use of exchange links in those sites.
Use auido clip search engines outside the United Stats. I used to use Chinese sites such as Baidu, Sogou, Yahoo China to search audio clips. Your browser maybe ask you to install simplified Chinese character, just ingore it. I always can find tons of English audio clips in those music search engines.
Use P2P software. It works well for full album audio clips specially. In fact, you almost can find everything with P2P software.
Visit artist's offical website. Some artists' sites provide mp3 files for fans to download.

Moyo wangu_Lyrics

Artist: Diamond
Song: Moyo wangu

(Chorous)
Moyo wangu..Moyo wangu mama..
Moyo wangu mimi umeniponza mamaa!
Moyo wangu,Moyo wangu mama,
Moyo wangu mimi umeniponza mamaa



(Verse one)
Upole wangu simanzi Eeeh!
Kwangu kupenda maradhi iiih!
Lakini kupendwaga mi nae bahati huwaga sina...
jichoni kwangu kibanzi Eeeeh!
ninakapenda kamanzi Iiih!
Oooh Licha ya kumthamini kama shilingi tatizo hata raha sina....
Ufinyu wa mboni zangu, unatazama mengi yanayonipa mateso,
Ukweli hatakupenda sina raha! ona nakonda kwa mawazo.
Masikini penzi langu jina lishakatwa na kauli roho inatoka kesho
Kutwa nzima mara Eeeh! Mara Iiiiii! Hata najuta kupenda....

(Chorous)
Moyo wangu..Moyo wangu mama..
Moyo wangu mimi umeniponza mamaa!
Moyo wangu,Moyo wangu mama,
Moyo wangu mimi umeniponza mamaa

(Vearse two)
Nikutwa kucha maneno,kosa si kosa maneno ilimradi tu karaha tantalila!
(Sina raha)
Ona sina tena mipango (aah ho aah!)
Kutwa nzima nnamawazo jina Mh!
aaaah! Sina raha Oooh! mama
Tamu ya wali ni nazi Eeeh!
Raha ya supu mandazi iiih!
Raha yangu me kupendwa tu naye lakini nyota sina.
Laana napata na radhi Eeeh! Nawakufuru wazazi iii!
Kwakung`ang`ana me kutaka kuwa nae lakini bahati sina!
Masikini roho yangu (roho yanguu) ingelikuwa ni nguo ningempa avae
Kkila kona akipita wamsifie ila lakini ni kikwazo
Masikini penzi langu jina lishakatwa na kauli roho inatoka kesho
Kutwa nzima mara Eeeh! Mara Iiiiii! Hata najuta kupenda

(Chorous)
Moyo wangu..Moyo wangu mama..
Moyo wangu mimi umeniponza mamaa!
Moyo wangu,Moyo wangu mama,
Moyo wangu mimi umeniponza mamaa x2

Monday, 24 September 2012

SIMULIZI YA MWEZI HUU- THE COMPANY MAN_MTU KAMPUNI

CHARACTERS:

Jovitha (Main)

john

Ali

Mama Jovitha

Mzee Joachim

Boazi

Pentlez

Jessi

Guest characters

Ande

Nkena

Atupilike

STORY STRUCTURE

Snake ( Middle, mouth to Tail)


LOCATION

Rwanda& Tanzania

(Sehemu zingine si sahihi bali ni za kufikirika

Kwa mf kolbert, K hospital n.k)


MAUDHUI

Mauaji

Rushwa

Tamaa

Ukiukaji wa sheria na haki za binadamu
UTANGULIZI
Jovitha ni Binti wa Kinyarwanda tena mzuri kupita kiasi kikubwa, kutokana na uzuri aliokuwa nao anawavutia wanaume wengi.Anaweza kujiunga na chuo kikuu cha Mzumbe akiwa anasomea sheria, anakuwa na uwezo mkubwa Darasani pamoja na kusumbuliwa na wanaume wengi kutokana na urembo wake tena wa kupitiliza ambao ulimvutia kila anayeitwa mwanaume.

Kutokana na uwezo wake mkubwa darasani anaweza kuwa na marafiki wengi. Pamoja na kuwa na Marafiki wengi pia kulikuwa na marafiki ambao ndani yake walikuwepo wanafiki, wanaomba urafiki ili watimilishe lengo lao na mwisho anafanyiwa unyama kwa kubakwa na wanaume zaidi ya 4 kwa lengo la kumkomoa hiyo yote ni kutokana na msimamo wake dhidi ya wanaume wengi walikuwa na tamaa naye.

Anahapiza kufanya kisasi, na anaanza kufanya mauaji ya kinyama….

Mwisho ambao ni mwanzo wa simulizi hii…Jovitha anaoneka uwanja wa ndege akiwa anaelekea UK kwa masomo zaidi kusomea digrii yake ya pili………ambapo ananguka kwa kuinusa sumu aliyowekewa na ALI. Anakimbizwa hospitalini ambako anaaga Dunia. Lakini jukumu anaachiwa kakae JOHN ili ahakikishe na kuuawa kwa ALI maana alihofia kuuangamizwa kwa familia yake.






SEHEMU YA KWANZA

Hali ya hewa ya Jiji kuu la nchi ya Rwanda Kigali ilikuwa shwali na likiwa na mwanga hafifu wa jua hali ambayo ilisabishwa kuwepo kwa wingu jeupe angani. Hali hiyo ilipendezesha jiji ilo ambalo likuwa linapendeza mno kwa hali ya ukijani wa mti inayoipamba Kigali. Lakini ndani yake alionekana Mrembo Jovitha. J akiwa anaelekea uwanja wa ndege Kolbert akiwa na Safari ya kuelekea masomoni UK –STANFORD UNIVERSITY, pamoja nakuwa na safari hiyo lakini kwake alikuwa hana raha kabisa mawazo yake yalikuwa juu ya Ali maana hakujua kama kweli kama amemmaliza kwani alihitaji kujua kama kweli amemaliza kazi yake juu ya kile alichoapa kuwamaliza waliombaka miaka miwili iliyopita.

Majira ya saa 2:00 asubuhi Jovitha tayari alikuwa uwanjani huku akisindikizwa na familia yake ambayo ilikuwa inaongozwa na kaka yake John kama kichwa cha familia baada yam zee Joachim kufa kwenye ajali mbaya ya moto akiwa kwenye gari yake. Wakati wote huo mama yake Jovitha alikuwa kimya kwani alionekana mwenye mawazo mengi, Jovitha alipoona ali hiyo kwa mama yake alimua kumsihi mama.

Mama punguza mawazo sawa, nakuomba sana” Jovitha alimwambia mama ake huku akimsogelea na kumukumbatia.

Sawa mwanangu nitafuata ushauri wako, Lakini mwanangu nitakuwa mpweke sana kwa kipindi chote cha masomo yako. Nakuomba uwe unanikumbuka pindi utakapokuwa masomoni” Mama Jovitha alimtazama motto wake kwa muda huku machozi yakimdondoka, kwa sasa alionekana wazi ya kwamba haitaji kutengana na Jovitha.

Hey Jovitha shughulika” punguza maongezi kwani hamchokani tu hata kumbikumbi uchokana pale mmoja atakapo toka mbawa” John alimuomba Jovitha huku akichomekea utani wake kama kawaida yake.

“Acha utani wako kaka, huyu ni mama siwezi kumchoka hata kidogo”Jovitha alijibu nakuongeza “Una maana gani unaposema hata kumbikumbi uchokana pale mmoaja atakapotoka mbawa”

“Aaaaah aah nina maana ya kwamba wewe bado una mbawa inakupasa uondoke na kutuachia mama yetu . maana mbawa zake zimetoka hivyo basi nawe zikitoka utatukuta chini ya aridhi hii ya Rwanda. Wewe ebu ruka salama sawa dada” john akaongeza huku akitania ndani yake ili mradi furaha ilejee ndani ya familia hii.

Jovitha aliiaga familia yake na baada ya Nusu saa alikuwa tayari amepanda ndege. Aliitafuta siti yake namba A25LD/1 ambayo ilikuwa Daraja la Kwanza akakaa huku akisubiri muda na kuiacha aridhi ya Kigali na kuelekea UK kwa masomo. Akiwa amekaa kwenye siti yake ametulia, mara akapita mhudumu akiwa ana Novels akiwagawia wasafiri. Mhudumu huyo alipofika kwenye siti aliyokaa Jovitha akatoa novel ya Harry Potter na kumpatia Jovitha aliyekuwa ameweka simu yake sikioni ni baada ya kupigiwa, akaipokea novel nakuiweka pembeni kwenye siti namba A24LD/1. Siti hii ilionekana haina mtu tangia Jovitha alipokaa hapo.

“hallo”Jovitha aliongea na simu

“hallo, how the day Jov” upande wa pili ukajibu

“Im fine, how you too n who am talking to?” Jovitha akajibu na uku akiuliza kama anaongea nani, kwani ilionekana wazi hakutambua anaongea na nani.

“Aaaaaaaaaah aaah, you’ve forgeten my voice? Just try to think 2 years before” upande wa pili ukaongea, uku ukisikika kwa sauti ambayo Jovitha angeiitambua wazi.

“No, who are you? Jovitha akazuga kwani hakutaka ieleweke kama katambua sauti ni ya nani.

“OK,let leave it. Open your novel page24 and don’t end your call” upande wa pili ukatoa maelekezo.

“Ok” Jane akajibu, akichukua kitabu chake alichopewa na kukifungua ukurasa alioelekezwa, alipofanikiwa kuupata ukurasa alishituka sana kwa alichokiona.

“Good by Jov, we shall meet again underworld sorry!!!!!!!!” upande wa pili ukamalizia na simu kukatwa.

“Tafadhali kila mmoja akae kwenye siti na kufunga simu zenu” ilikuwa sauti ya mhudumu mmoja kwenye ndege ikiwa ni ishara ya ndege kuacha aridhi ya Kigali.

Jovitha akiwa amedua kwa muda kwa kile alichokiona, hakuamini macho yake. Mara ghafla jasho jingi kama mfereji wa maji yakamtoka. Akanyanyuka kwenye siti kwa lengo kupata maji ili aweze kunawa uso wake uliojaa jasho kwa kipindi kifupi tu, lakini aliponyanyua hatua mbili za miguu yake akaanguka chini huku akiwa na povu jingi mdomoni likiambatana na damu ambayo ilianza kutoka puani.

“Hallo kapteini tunaomba ndege irudishe kuna tatizo kidogo” mawasiliano yakapelekwa kwa kapiteni wa ndege hiyo.

“Tatizo gani?” kapiteni akauliza.

“kuna mwana dada kaanguka huku daraja la kwanza” mhudumu huyo wa ndege akajibu.

“sawa”kapiteni akakubali kurudisha ndege, kwa kuwa ilikuwa bado kuacha aridhi,

Na hiyo ilikuwa ni baada ya kutoa taarifa kwa waongozaji wa ndege.

“Mmmmh nani tena huyu?” mmoja wa abiria akasikika akiuliza swali. Wakati huo Jovitha akiwa anagalagala chini, hakuwa na uwezo wa kuona zaidi ya kuona kwa shida.

Jovitha” mhudumu mmojawapo akajibu kwa mkato.

“kutoka wapi? Na kwa nini kaanguka mahali hapa?” akaongeza swali lingine ambalo alikupata kujibiwa na yeyote bali watu wote wakageuka na kumuangali muuliza swali tena kwa macho makali, ambapo hadi alipojishitukia mwenyewe kisha kuona haibu na kuondoka eneo hilo.

Jovitha akanyanyuliwa na kuwekwa kwenye machela ambapo alipakiwa kwenye gari la kubebea wagonjwa na ni baada ya kumpa huduma ya kwanza. Baada ya dakika mbili tu ikaanza safari ya kumpeleka hosipitali ya K Hospital ya Jijini Rwanda.

****************************************************************************

Gari la kubebea wagonjwa lilionekana likiwa kasi likikatisha mitaa ya Kigali Road kuelekea K Hospital likiwa karibu kulifikia Daraja la Dotown Bridge. Gari lilipofika karibu kabisa na Daraja Navjay ambaye alikuwa dereva alishangazwa kuwepo kwa watu walioshikiria Binduki mikononi wakiwa wamekaa kwa mashambulizi. Baada ya dreva kuona dalili hiyo akawaagiza wenzake ili wamlinde mgonjwa wao, Jovitha kwa taabu sana alisikia Dereva akiongea ya kwamba ahakikishiwe ulinzi zaidi.
Dereva alivuta mafuta zaidi kuakikisha anavuka kizingiti icho kwani alitambua hao watu hawana amani kabisa. Kweli alivyofikiria ndivyo ilivyokuwa kwani watu hawa walianza kumimina risasi kuelekea wao na risasi nyingi kumpata dereva huyo lakini hakukata tama kabisa, lengo likiwa kuvuka kizingiti na kwa bahati akavuka.
ITAENDELEA
futilia wiki ijayo

Monday, 10 September 2012

somalia wapata rais mpya

Bunge la Somalia limemchagua
Hassan Sheikh Mohamud kuwa Rais
mpya wa nchi hiyo.
Kulikuwa na wagombea 22 kwenye
uchaguzi huo, akiwemo Rais
anayeondoka Shariff Sheikh Ahmed
na waziri mkuu Abdiweli Mohamed
Ali.
Hassan Sheikh Mohamud alishindat
kufuatia duru ya tatu ya upigaji kura,
ambapo alikuwa anachuana na Rais
anayeondoka Shariff Sheikh Ahmed.
Katika raundi ya kwanza Sheikh
Ahmed alikuwa amepata ushindi
mwembamba wa kura 64 dhidi ya 60
alizopata Sheikh Mohamud.
Kwa jumla wabunge 271 walipiga
kura.
Katika duru ya mwisho wabunge
wengi waliowaunga mkono
wagombea waliochujwa walimuunga
mkono Sheikh Mohamud , akapata
kura 190 dhidi ya 70 alizopata Rais
anayeondoka.
Hii ni mara ya kwanza kwa uchaguzi
wa Rais kufanyika katika mji mkuu wa
Somalia Mogadishu, tangu
kuondolewa kwa serikali ya kijeshi
mwaka 1991.

Wednesday, 22 August 2012

Sitta:Msiisubiri Serikali kutaja walioficha mabilioni

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta AWASHANGAA WANAOIPA MUDA HUKU WAKIWAFAHAMU WAHUSIKA, ASEMA HAIWEZEKANI MWANASIASA KATIKA NCHI MASKINI AWE BILIONEA, ATAKA WAKAMATWE WAFIKISHWE MAHAKAMANI

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta amewataka wanaotangaza kuwafahamu vigogo walioficha mabilioni ya fedha nje ya nchi kuwataja mara moja ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao badala ya kuisubiri Serikali kufanya hivyo.Kauli hiyo ya Sitta ambaye pia ni Mbunge wa Urambo Mashariki (CCM), imekuja wakati baadhi ya wanasiasa, wakiwamo wabunge kutishia kuwataja watu hao, lakini wakisisitiza kuwa ni pale tu Serikali itakaposhindwa kufanya hivyo.

Utafiti uliofanywa na Shirika la Kimataifa la Fedha la Global Financial Integrity, unaonyesha kuwa tatizo la utoroshaji wa fedha nchini limekuwapo katika awamu zote za Serikali zilizoiongoza Tanzania, lakini Awamu hii ya Nne imetia fora.

Utafiti huo uliofanywa kuanzia mwaka 1970 hadi 2009, unaonyesha kuwa katika utawala wa Rais Jakaya Kikwete, fedha zilizofichwa nje ya nchi ni Dola za Marekani 7,967.4 milioni (sawa Sh12.7 trilioni).

Akizungumza katika mahojiano maalumu, kuhusu nini kifanyike ili kuiokoa Tanzania isiendelee kufilisiwa na watu wachache, Sitta alisema anasikitishwa na watu hao kuogopa na kuwaficha watu wanaofisadi mali za nchi na hasa pale inapokuwa wahusika ni vigogo wa Serikali.

Alisema vigogo hao ni sababu ya watu kupata kigugumizi katika hili akihoji : “Kwa nini linapokuwa ni suala linalowahusu hawa wanaoitwa vigogo hawatajwi?”

Sitta ambaye ameshika nyadhifa mbalimbali serikalini katika awamu tofauti, alisema haoni kama kuna kosa kumtaja hadharani mtu aliyeficha fedha nje ya nchi huku akisababisha Watanzania kuendelea kukabiliwa na maisha magumu.

“Watajwe! Kama ni Samuel Sitta ameficha fedha nje atajwe. Kwa kweli mimi sioni kama kuna dhambi yoyote kumtaja,” alisema Sitta huku akisisitiza kwamba huo ni msimamo wake binafsi unaotokana na uzoefu wake kwenye uongozi wa nchi na siyo kwa mamlaka aliyonayo ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Alisema njia nzuri ya kukomesha tabia hiyo ni kuwataja na vyombo husika kuwafikisha mahakamani kwa kuzingatia kuwa sheria ni msumeno, haipaswi kubagua aliye mdogo au mkubwa kwa maana ya wadhifa katika nchi.Sitta ambaye pia aliwahi kuwa Spika wa Bunge alisema: “Swali la kwa nini hawatajwi, ni jambo la kushangaza.”

Alisema amesikia na kuwasoma baadhi ya wanasiasa wakitishia kuwa watawataja wahusika iwapo Serikali haitafanya hivyo, lakini akasema haoni sababu yoyote ya mtu kusita katika kuokoa taifa dhidi ya wizi wa fedha za umma.

“Haiwezekani kwa mwanasiasa yeyote katika nchi maskini kama Tanzania au kiongozi wa Serikali kuwa na utajiri wa mabilioni ya fedha.”

Alisema hata kama anafanya biashara, siyo rahisi kuwa na utajiri wa kiwango hicho hasa ikizingatiwa kuwa hutumia muda mrefu kulitumikia taifa.“Sisi tunaofanya kazi serikalini, tunatoka saa moja usiku. Sasa muda huo wa kufanya biashara ni saa ngapi?”

Tuhuma hizo ziliibuka bungeni Jumatano iliyopita baada ya Kambi ya Upinzani kudai kwamba nawafahamu wahusika wa ufisadi huo na kutishia kuwataja ikiwa Serikali haitafanya hivyo.

Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Zitto Kabwe alipokuwa akiwasilisha hotuba ya kambi yake kuhusu Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Fedha alisema miongoni mwa wanaomiliki fedha hizo ni kiongozi wa juu nchini pamoja na aliyepata kuwa waziri katika Serikali ya Awamu ya Tatu iliyoongozwa na Benjamin Mkapa.


Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili ulibaini kwamba kuna Watanzania 27, wakiwamo wanasiasa na wafanyabiashara walioficha mabilioni ya fedha huko Uswisi, huku mmoja wao akiwa anamiliki Dola za Marekani milioni 56 (sawa na Sh89.6 bilioni).

Katika uchunguzi huo ilibainika pia kuwa kiasi cha fedha kilichothibitishwa kumilikiwa na Watanzania hao ni jumla ya Dola za Marekani 186 milioni (takriban Sh300 bilioni) kwa viwango vya sasa vya kubadilishia fedha ambavyo ni Sh1,600 kwa Dola ya Marekani.

Taarifa hizo zinaeleza kuwa mbali na kigogo anayemiliki Sh90 bilioni, wapo wengine wanne huku anayefuatia akiwa anamiliki Dola 30 milioni (Sh48 bilioni), mwingine dola 20 milioni (Sh32 bilioni) na wengine wawili kila mmoja anamiliki dola milioni 10 (Sh16 bilioni).


Hiyo inamaanisha kwamba vigogo watano tu katika kundi hilo, wanamiliki Dola milioni 126 (Sh201.6 bilioni) sawa na asilimia 67.74 ya fedha hizo, wakati wengine 22 waliobaki wanamiliki Dola milioni 60 (Sh96 bilioni) sawa na asilimia 32.25.

Kwa hesabu za kawaida, kiasi cha Sh300 bilioni, kinaweza kugharimia ujenzi wa vyumba vya madarasa zaidi ya 33,300, ikiwa chumba kimoja kinagharimu kiasi cha Sh9 milioni.

Katika orodha ya walioweka fedha nchini humo, pia wamo wafanyabiashara wanaomiliki kiasi cha dola kati ya milioni mbili na milioni saba. Kadhalika, wamo wawili waliowahi kuwa mawaziri katika Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Mwalimu Julius Nyerere ambao akaunti zao zina kiasi kisichozidi Dola 500,000 kwa kila mmoja

LATEST NEWS

Share

Widgets

 

Total Pageviews