Social Icons

Tuesday 19 June 2012

WEMA SEPETU ANAJIAIBISHA SASA!!

Hivi karibuni baada ya kutokelezea na kipindi cha Take one cha clouds Tv akionesha nyumba yake mpya aliyonunua kwa zaidi ya Tsh. milioni 400 kijitonyama huku akiendelea na kutuonesha baadhi ya magari yake anayomiliki sasa hali imegeuka na kuwa ggumzo hapa Tanzania. Baada ya kuonesha baadhi ya vitu vilivyomo ndani humo na kudai kuwa nyuma hiyo ni yake na ameitengeneza kwa pesa zake, kimeibuka kisanga kingine baada ya kuibuka kwa

wapambe na mmiliki wa nyumba hiyo ambaye ni Mama mtu mzima na kuweka wazi kuwa nyumba hiyo si ya Wema bali amepangishiwa na amelipiwa kiasi cha miezi sita na mtu aliyedaiwa kuwa ni mpenzi wake na pia bado anadaiwa kiasi kingine cha miezi sita. Na hii kama itakuwa ni kweli basi hawa wanaojiita mastaa wetu wa Bongo hawatakuwa na la maana zaidi ya kujidharirisha,kama kitu si chako kwanini usiweke wazi!!.


No comments:

LATEST NEWS

Share

Widgets

 

Total Pageviews