Social Icons

Thursday 1 March 2012

MVUA YA UPEPO MKALI YANYESHA WILANI KYELA

Mvua iliyoambatana na kimbunga ilizonyesha jana ya tarehe 29 februari imesababisha maafa hapa wilayani, karibia nyumba nyingi zimeezuliwa mabati likiwemo kanisa kubwa la morovian lililopo kijiji cha Ibungu. Habari ikiripotiwa toka eneo lililopo kanisa hilo nami nikiwa shuhuda wa tukio hilo ni kwamba tatizo kubwa lililosababisha kanisa kuezuliwa ni kwasababu ya kutomaliziwa kwa  madirisha yake. Baada ya tukio hilo niliweza kukuta na Mchungaji Mzee Mwakyalo alisema yeye binafsi anasikitishwa sana na kuezuliwa kwa kanisa hila alisisitiza ya kwamba kila mtumishi wa kanisa hilo aweze kuvumilia hali iliyotokea kwani ni mipango ya mungu.
Mimi binafsi niliweza kusikitishwa na hali ya hewa iliyotokea siku ya jana, lakini ningelipenda kusisitiza hili la kuezuliwa kwa kanisa hili, tatizo sio tu la madirisha kutokamilika bali ni “ukwasi”. Kwani hili ndilo tatizo kubwa la makanisa yaliyopo vijijini kwani vijana na wazee ambao niwaumini wa makanisa hayo huwa wanajituma sana kufyatua tofali za kujengea makanisa hayo lakini mwisho makanisa mengi huanguka na kuwa magofu. Jambo la muhimu kwa makanisa haya ambayo yana maaskofu na viongozi mbalimbali wasiangaliwe huduma hii kwa undani bila kusahau vijijini na sikuangalia mijini tu ambako ndiko viongozi wetu wa dini wanakojenga makanisa huku wengi wakidai nikutokana naongezeko la watu na kuifanya huduma kumfikia kila mtu.
Wakati huohuo katika eneo la mikumi imeripotiwa kuvunjika tawi la mti na kuua ng’ombe mmoja, pia maeneo  mbalimbali kumetokea uharibifu mkubwa wa mazao kama migomba na mahindi kuanguka.

No comments:

LATEST NEWS

Share

Widgets

 

Total Pageviews