Rais Jakaya Kikwete
amechaguliwa na kushinda kwa kishindo uchaguzi wa nafasi ya Mwenyekiti wa CCM
taifa kwa kupata kura 2395.kati ya 2397 zilizopigwa hii leo. Kwa matokeo hayo
Ndugu Jakaya Kikwete ameitetea vyema nafasi yake hiyo hadi mwaka 2017. Huku kura
za hapana zikiwa 2. Sawa na asilimia 99.92.
Aidha wagombea wa Nafasi
ya Makamu Mwenyekiti ambazo kwa upande wa Bara ilikuwa ikigombewa na Katibu Mkuu
wa zamani wa CCM, Philip Mangula na amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM
Bara kwa kura 2397, huku nafasi ya Makamu Mwenyekiti Zanzibar ameshinda Raius
wa Zanzibar, Dk.Ali Mohamed Shein kwa kupata kura zote zilizopigwa 2397. Ushindi
wa Shein na Mangula kushinda kwa kura za Ndio kwa Asilimia 100
No comments:
Post a Comment