Social Icons

Tuesday 7 February 2012

NALO HILI MUHIMU, KUUTAZAMA ULIMWENGU !


  •    BARACK OBAMA, RAIS WA MAREKANI
“Kuwa Rais kunamsukuma aone uhitaji wa kusali”- Katika hili tunamhitaji kiongozi mwenye misingi ya dini na mwenye kuamini.

  • ·        LA NACION, ARGENTINA
“Walipoulizwa wachague njia ya kuonyesha uzalendo wao, asilimia 56 ya waargentina wenye umri wa kati ya miaka 10 na 24 walisema kwamba wangependa kuvalia jezi ya timu ya kandanda ya Taifa”.-. Hapa kuna jambo la msingi tunaweza kujifunza watanzania. Je sisi kama wazalendo watimu yetu ya Taifa, hili kwetu tumekuwa waraibu tuko tayari kuvaa jezi ya Brazil nakuacha jezi zetu.

  • ·        SHIRIKA LA CHAKULA NA KILIMO LA UMOJA WA MATAIFA, ITALIA.
Matokeo ya utafiti Fulani yalidokeza kwamba “inakadiriwa kwamba asilimia 33 ya chakula kinachozalishwa ulimwenguni pote kwa ajili ya wanadamu hupotea au kutupwa, na hiyo ni kama jumla ya tani bilioni 1.3 kwa mwaka”

  • ·        PATRIARRCH KRILL, MKUU WA KANISA LA OTHODOKSI LA URUSI.
Siku hizi, vita na ripoti za vita zimeenea ulimwenguni pote kwa mfano Misri, Libya Somalia n.k, kwa hiyo jeshi la nchi yetu lazima liwe tayari siku zote kuwalinda watu wake na kila kitu ambacho tunaona kuwa ni kitakatifu kutokana na maadui wanaotoka nchi nyingine.

  • ·        PRESSEPORTAL, UJERUMANI.
Kiwango cha juu cha kabisa aksidenti za magari kilichoripotiwa kwa kampuni moja ya bima nchini ujerumani katika mwaka wa 2010, kilionesha kwamba aksidenti hizo zilitokea kati ya saa mbili asubuhi. “Mojawapo ya njia muhimu zaidi ya kuzuuia aksidenti ni kuwa na wakati wa kutosha wa kusafiri unapoelekea kazini asubuhi,” anasema afisa wa kampuni hiyo.

No comments:

LATEST NEWS

Share

Widgets

 

Total Pageviews