- BARACK OBAMA, RAIS WA MAREKANI.
“Kuwa
Rais kunamsukuma aone uhitaji wa kusali”- Katika hili tunamhitaji kiongozi
mwenye misingi ya dini na mwenye kuamini.
- · LA NACION, ARGENTINA
“Walipoulizwa
wachague njia ya kuonyesha uzalendo wao, asilimia 56 ya waargentina wenye umri
wa kati ya miaka 10 na 24 walisema kwamba wangependa kuvalia jezi ya timu ya
kandanda ya Taifa”.-. Hapa kuna jambo la msingi tunaweza kujifunza watanzania.
Je sisi kama wazalendo watimu yetu ya Taifa, hili kwetu tumekuwa waraibu tuko
tayari kuvaa jezi ya Brazil nakuacha jezi zetu.
- · SHIRIKA LA CHAKULA NA KILIMO LA UMOJA WA MATAIFA, ITALIA.
Matokeo
ya utafiti Fulani yalidokeza kwamba “inakadiriwa kwamba asilimia 33 ya chakula
kinachozalishwa ulimwenguni pote kwa ajili ya wanadamu hupotea au kutupwa, na
hiyo ni kama jumla ya tani bilioni 1.3 kwa mwaka”
- · PATRIARRCH KRILL, MKUU WA KANISA LA OTHODOKSI LA URUSI.
Siku
hizi, vita na ripoti za vita zimeenea ulimwenguni pote kwa mfano Misri, Libya
Somalia n.k, kwa hiyo jeshi la nchi yetu lazima liwe tayari siku zote kuwalinda
watu wake na kila kitu ambacho tunaona kuwa ni kitakatifu kutokana na maadui
wanaotoka nchi nyingine.
- · PRESSEPORTAL, UJERUMANI.
Kiwango
cha juu cha kabisa aksidenti za magari kilichoripotiwa kwa kampuni moja ya bima
nchini ujerumani katika mwaka wa 2010, kilionesha kwamba aksidenti hizo
zilitokea kati ya saa mbili asubuhi. “Mojawapo ya njia muhimu zaidi ya kuzuuia
aksidenti ni kuwa na wakati wa kutosha wa kusafiri unapoelekea kazini asubuhi,”
anasema afisa wa kampuni hiyo.
No comments:
Post a Comment