LEO hii karibia asilimia kubwa ya wanafunzi wa chuo kikuu
cha Udom wafanya mitihani yao ya mwisho ya semista gizani, hii nikutokana na
kukatika kwa umeme, ili limewatokea wanafunzi wale ambao walikuwa na mitihani
jioni ya usiku huu wa tarehe 17 februari na wengi wao walikuwa ni wale wa mwaka
wa tatu.
Wakati hili likitokea utawala wa chuo waliamua kutoa
taarifa TANESCO , ambao walihaidi kurudi kwa umeme baada ya dakika chache,
walimu wa kozi husika walitoa angalizo kwa wanafunzi
kwamba wasubiri umeme utarudi lakini haikuwa hivyo walivyotarajia kwani umeme haukurudi kwa wakati. Ndipo ulichukuliwa uhamuzi wa walimu kwamba wanafunzi ambao hawakumaliza mitihani waweze kukusanya mitihani na vijitabu vya kujibi mitihani ili kurinda hadhi ya mitihani na kuepuka uhalisia wa mitihani hiyo(validity and reliability of exams) kwa kweli huo ndio ukweli halisi maana giza lilianza kuwa kubwa kwenye vyumba vyote vya mitihani. Ndipo wanafunzi walipoweza kukusanya mitihani na vijitabu vya kujibia mitihani.
kwamba wasubiri umeme utarudi lakini haikuwa hivyo walivyotarajia kwani umeme haukurudi kwa wakati. Ndipo ulichukuliwa uhamuzi wa walimu kwamba wanafunzi ambao hawakumaliza mitihani waweze kukusanya mitihani na vijitabu vya kujibi mitihani ili kurinda hadhi ya mitihani na kuepuka uhalisia wa mitihani hiyo(validity and reliability of exams) kwa kweli huo ndio ukweli halisi maana giza lilianza kuwa kubwa kwenye vyumba vyote vya mitihani. Ndipo wanafunzi walipoweza kukusanya mitihani na vijitabu vya kujibia mitihani.
Baada ya muda mchache umeme ukarudi na ni baada ya
wanafunzi kutoka, wakati huo huo chuo cha elimu tatizo lilikuwa hilo hilo,
ampapo inaripotiwa ya kwamba umeme ulipo rudi kama nusu saa hivi Tangazo
lilitolewa ya kwamba kwa wale wanafunzi walioweza kufanya mtihani wa “utafiti
katika elimu” ya kwamba wasiondoke na kwenda makwao hadi uamuzi utakapo
chukuliwa wa nini kifanyike. Lakini hadi sasa wanafunzi wengi wameweza kuondoka
chuoni hapo na hiyo ni baada ya kutoka kwenye mtihani na pia na wengine
wanategemea kuondoka hasubuhi kwani wengi wao waliweza kukata tiketi mapema kwenda
makwao, hadi dakika ya mwisho chanzo cha habari hizi kinasema wanafunzi wengi
hawakubaliani na tangazo hilo maana wengi wao tayari wameshaondoka na hawapo
tena chuoni na wengine wameishakata tiketi tayari kwa safari.
Lakini penye jambo pia kuna ukinzani wengine walitoa
mapendekezo ya kwamba mitihani yote iliyofanyika muda huo iweze kurudiwa
wamependekeza hivyo.wamesema haina budi kufanya hivyo pamoja na kwamba ni
gharama kubwa kurudia na kukidhi gharama za mitihani hiyo.
Hadi tunafikia tamati, jibu la nini kifanyike halijulikani
hadi uamuzi kamili utakapo tolewa kesho na wakuu wa idara husika.
No comments:
Post a Comment