Shirika la kutetea haki za binadamu Human Rights
Watch limesema kuwa shughuli ya uchimbaji dhahabu kaskazini mwa Nigeria
imewasababishia maelfu ya watoto maradhi mabaya zaidi kutokana na
uchafuzi wa madini ya chuma.
Human Rights Watch inasema kuwa uchafuzi huo
ndio mbaya zaidi kuwahi kutokea katika miaka ya hivi karibuni na watoto
wengi katika eneo hilo wanahitaji msaada wa kimatibabu. Shirika hilo linasema tayari watoto mia nne wamekwishaaga dunia kutokana na mkasa huo. Baadhi ya watoto hao ambao wana umri wa miaka minane wanafanya kazi katika migodi ya dhahabu katika jimbo la Zamfara.
Viwango vya uchafuzi wa madini ya chuma ni vya juu zaidi katika
baadhi ya vijiji na takriban asilimia arobaini ya watoto walioenekana
kuwa na dalili ya kupata maradhi yanayotokana na uchafuzi huo wameaga
dunia. Shirika la Human Rights Watch linasema kuwa
uchimbaji wa madini unawaweka watoto hao katika hatari ya kuathirika na
vumbi ya madini hayo ya chuma ambayo inachafua maji pamoja na chakula. Shirika la afya duniani WHO linasema kuwa madini ya chuma husababisha matatizo ya kudumaa ubongo na umbo la watoto.Read More
No comments:
Post a Comment