Kwa muda sasa,hali ya afya ya Naibu Waziri wa Ujenzi na Mbunge wa
Jimbo la Kyela mkoani Mbeya,Dr.Harrison Mwakyembe, imekuwa ni gumzo
lisiloisha.Yanasemwa mengi kuhusu ugonjwa unaomsumbua.Yeye mwenyewe
hajaweka bayana juu ya ugonjwa wake.Serikali nayo,kwa kuzingatia
taratibu za kitabibu,haiwezi kusema kitu.Bado anaugua.
Pamoja na kwamba bado anaugua,hali yake inaendelea vizuri.Mwishoni
mwa wiki alithibitisha hilo pale alipoweza kuhudhuria ibada katika
Kanisa la Ufufuo na Uzima linaloongozwa na Mch.Josephat Gwajima lililopo
maeneo ya Kawe jijini Dar-es-salaam.
No comments:
Post a Comment