BENKI ya CRDB imekabidhi sh milioni 5, kwa Shule ya Sekondari ya Minaki ili zitumike kwa ajili ya kuendeleza elimu shuleni hapo. Msaada huo ulitolewa jana na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo,
Dorah Ngarija, wakati wa mahafali ya 52 ya shule hiyo, akisema kiasi
hicho kimetolewa kwa lengo la kutatua baadhi ya kero zinazoikabili shule
hiyo.
Alisema benki hiyo imekuwa ikitoa mchango mkubwa kwa sekta ya elimu,
ikiwemo ya kutoa mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ili
kupata uzoefu wa kikazi.
Dorah alisema CRDB imefanikiwa kuwapelekea huduma za kibenki
wanafunzi wa elimu ya juu ili waendelee kupata huduma za fedha wakiwa
vyuoni.
Aliutaka uongozi wa shule hiyo kuendeleza historia iliyoachwa ya kuwa
chanzo cha kutoa wanafunzi ambao baadaye watakuwa viongozi bora wa
baadaye. Awali, mkuu wa shule hiyo, Arnold Chungu, alisema licha ya shule hiyo
kuwa kongwe inakabiliwa na changamoto mbalimbali kama uhaba wa vifaa,
maji safi na salama ya kunywa.
Source: Tanzania Daima
No comments:
Post a Comment