Juzi ya tarehe 23 ya mwezi February,
2012 mida ya saa 1 usiku mpaka saa 5 na nusu usiku katika eneo la Mwenge Vinega
wa anti virus tulikutana katika kufanya tathmini na kujadli maridhiano ya
kumaliza ugomvi wa kimaslahi kati ya Kundi la Vinega na Redio Clouds pamoja na
Bwana Rugemalila Mutahaba,katika kikao hicho tuliridhiana kutoa tamko hili kwa
umma wote wa watanzania na wapenda maendeleo wote wa sanaa yetu.
"Ni kweli hakunaga Vita isiyo na mwisho lakini pia katika kila vita malengo ya msingi yanapaswa kuwa mbele na daima mbele...Harakati hizi za Anti virus zilipoanza wengi tulionekana kama wasaliti na wapuuzi,wahuni na kuonekana kama tuna wivu tu na mafanikio ya baadhi wa wadau ila daima tulisimama katika kweli na hatimae Umma/jamii ya watanzania ukasikia sauti na hoja zetu na kuona kweli tuna mambo ya msingi,Hoja zetu mbele ya umma ndio ilikuwa silaha ya vita hii ya Anti virus na wala si nguvu ya Propaganda na uzushi...Tumepiga makelele na hatimaeTaifa zima wakaona kweli hapa kuna hoja na zinapaswa kuzingatiwa na wala si ugomvi wa mtu mmoja bali ni harakati za kweli za kukomboa sanaa yetu na kuvunja ile mifumo ambayo siyo sahihi inayoendelea kunyonya jasho la wasanii wa Tanzania na kuwafanya kuwa mafukara na wasio na mategemeo na kupelekea kujiingiza katika matumizi ya madawa ya kulevya na hatimae kufanya mambo ya kihalifu.Sanaa hii kwa muda imekuwa ikihodhiwa na watu wachache na kujitajirisha na kuacha lundo la wasanii kuishi maisha mabovu.Dhamira yetu ni kumaliza kabisa mifumo hii mibovu ambayo tunaamini ikimalizwa msanii wa kitanzania ataweza kupata kipato na kujiajiri na kuendesha maisha yake sawasawa.
"Ni kweli hakunaga Vita isiyo na mwisho lakini pia katika kila vita malengo ya msingi yanapaswa kuwa mbele na daima mbele...Harakati hizi za Anti virus zilipoanza wengi tulionekana kama wasaliti na wapuuzi,wahuni na kuonekana kama tuna wivu tu na mafanikio ya baadhi wa wadau ila daima tulisimama katika kweli na hatimae Umma/jamii ya watanzania ukasikia sauti na hoja zetu na kuona kweli tuna mambo ya msingi,Hoja zetu mbele ya umma ndio ilikuwa silaha ya vita hii ya Anti virus na wala si nguvu ya Propaganda na uzushi...Tumepiga makelele na hatimaeTaifa zima wakaona kweli hapa kuna hoja na zinapaswa kuzingatiwa na wala si ugomvi wa mtu mmoja bali ni harakati za kweli za kukomboa sanaa yetu na kuvunja ile mifumo ambayo siyo sahihi inayoendelea kunyonya jasho la wasanii wa Tanzania na kuwafanya kuwa mafukara na wasio na mategemeo na kupelekea kujiingiza katika matumizi ya madawa ya kulevya na hatimae kufanya mambo ya kihalifu.Sanaa hii kwa muda imekuwa ikihodhiwa na watu wachache na kujitajirisha na kuacha lundo la wasanii kuishi maisha mabovu.Dhamira yetu ni kumaliza kabisa mifumo hii mibovu ambayo tunaamini ikimalizwa msanii wa kitanzania ataweza kupata kipato na kujiajiri na kuendesha maisha yake sawasawa.